Msanii marufu toka Tanga Bwana Misosi aliyetamba zamani na wimbo wake wa MABINTI WA KITANGA ametoa tarifa kuawa account yake ya FACEBOOK imeingia mikononi mwa wajanja (Hackers). Misosi alipata ujumbe kutoka kwa mtu akimlazimisha abonyeze link ambayo ilianza na maneno ya kuwa ameandikwa vibaya kwa habari kamili bonyeza hiyo link. Misosi akabonyeza wakati anaendelea ukaja ujumbe eti aingize email yake na password ili auone huo upuuzi, basi ndugu yetu akaingiza mwisho wa siku jamaa wakaendelea kufanya yao. Sasa Bw Misosi anawaomba mashabiki wake kutoingia kwenye account yake hii https://www.facebook.com/bwana.misosi au ukiona vitu vya upuuzi usiamini kuwa ni yeye.
Ushauri wangu wa bure kwa wasanii wa hapa nyumbani msipende kubonyeza bonyeza link mtakazotumiwa yasije kuwakuta kama yaliyomkuta ndugu yetu Bw. Misosi. Kuna link na link unaweza kubonyeza sasa mpaka link hii inasema weka email yako na Password bado tu unaendelea kujaza mmmmh hii ni zaidi ya noma.
0 comments:
Post a Comment